RAIS MAGUFULI AAGIZA NDEGE ZA RAIS ZIANZE KUBEBA ABIRIA

Rais Dkt. Magufuli ameagiza kwamba ndege 2 kati ya ndege 3 za Rais, zipakwe rangi ya Air Tanzania na zianze kutumika kusafirisha abiria.

Ametoa agizo hilo jana Ijumaa Januari 11, 2019 wakati wa mapokezi ya ndege ya pili aina ya Airbus A220-300 iliyowasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.

“Kwa kuwa rais mwenyewe hasafiri hovyo sasa zinakaa kufanya nini na moja ina uwezo wa kubeba watu 50. Hii haitabeba abiria pale tu ambako itakuwa inatumika,” amesema Rais Magufuli.

Akijibu ombi la Askofu mkuu wa kanisa la Full Gospel Bible fellowship (FGBF) Zachary Kakobe aliyemuomba kuwa na desturi ya kukutana na viongozi wa vyama vya siasa kama ilivyo kwa viongozi wa dini, Magufuli amesema anaogopa kukutana na watu ambao wanatukana na kutishia kumkatakata.

“Huwezi kukutana na mtu anayekuambia akikushika atakukata halafu ukutane naye kumbe ndiyo siku yako ya kuchinjwa hivyo ni bora umuache akae mwenyewe huko,” amesema Rais Magufuli

Aidha Rais Magufuli ameshwashukuru wabunge wa Chama cha Mapinduzi kwa kuwezesha maendelo hayo kupitia kuunga kwao mkono bajeti inapopelekwa bungeni.

Airbus 220-300 imekuwa ni ndege ya 6 kuwasili nchini miongoni mwa 7 zilizonunuliwa na Serikali huku nyingine moja ikisubiriwa ambapo leo Rais amethibitisha kuwa ndege nyingine ya 8 inanunuliwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527