WAUZA MADINI WALIVYOIBA BENKI KUU

Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernard Y. Kibesse.

Dkt. Kibesse ameyasema hayo leo Jijini Dar es salaam, katika Mkutano wa wachimbaji, Wafanyabiashara na Wadau wa sekta ya madini nchini.

Awali kabla ya kujibu swali la Rais Magufuli ambaye aliuliza BOT imejipangaje licha ya kuwa hapo nyuma ilikuwa ikishirikiana na wauzaji wanaoibia serikali.

Dkt. Kibese amesema kwamba Benki Kuu haina tatizo na kununua dhahabu, hapo awali mpaka mwaka 1994 BoT ilikuwa ikinunua dhahabu, "taifa lenye watu wasio waaminifu, haliwezi kuwa Taifa endelevu, kilichotukuta tuliuziwa dhahabu feki tukaamua kusimamisha ununuzi".

Ameongeza kuwa, "Tunafahamu kuwa 'Reserve' za Benki Kuu nyingi duniani zinakuwa na hazina za dola na dhahabu, nasi tunaweza lakini tupo tayari kuanza kununua tena. Tunaelewa Benki Kuu nyingi zinakuwa na hazina ya dhahabu".

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527