SIMBA KUSAJILI WACHEZAJI WAWILI KUTOKA MAGHARIBI

Mchezaji Lamine Moro kutoka Ghana.

Taarifa ya klabu hiyo leo imeeleza kuwa wachezaji walioletwa ni wa eneo la ulinzi na ushambuliaji ambao wanatoka mataifa ya Ghana na Togo na watasajiliwa endapo kocha Patrick Aussems ataridhishwa na kiwango chao.

''Wachezaji Lamine Moro kutoka Ghana (beki) na Hunlede Kissimbo Ayi-Abel kutoka Togo (mshambuliaji) wamejiunga na timu yetu kwa majaribio'', imeeleza taarifa hiyo.

Aidha taarifa imefafanua kuwa iwapo Kocha Mkuu Patrick Aussems ataona wanafaa kuwatumia katika mashindano yanayoikabili timu hiyo watasajiliwa.

Tetesi zinaeleza kuwa endapo nyota hao watafuzu italazimika wachezaji wawili wa kimataifa wawili waachwe huku Pascal Wawa na Juuko Murushid, tetesi zinaeleza kuwa wanaweza kuachwa katika eneo la ulinzi.

Simba tayari ina wachezaji 10 wa kimataifa ambao ndio wanatambulika kwa mujibu wa kanuni za TFF hivyo hawaruhusiwi kuongeza.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527