KAMBI YA KABILA YAKANUSHA KUHUSU MIKUTANO YA MAKABIDHIANO YA AMANI YA MADARAKA

Timu ya Kampeni ya mgombea urais nchini Congo Felix Tshisekedi, imesema wawakilishi wa kambi yao wamekutakana na kambi ya rais anaemaliza muda wake Joseph Kabila kuhakikisha makabidhiano ya amani ya madaraka.


Kambi ya Kabila hata hivyo imekanusha kuwepo na mikutano kama hiyo tangu kufanyika kwa uchaguzi wa Desemba 30, ambao matokeo yake ya awali yanatarajiwa kutangazwa baadae wiki hii.

Uchaguzi huo ulinuwia kuleta mabadiliko ya kwanza ya kidemokrasia nchini Congo katika kipindi cha miaka 59 ya uhuru wake, lakini wasiwasi unazidi kuenea huku baadhi ya wanasiasa wa upinzani wakiituhumu serikali kwa kujaribi kuiba kura.

Matokeo mengine yanayobishaniwa huenda yakazusha aina ya vurugu zilizoshuhudiwa baada ya uchaguzi wa mwaka 2006 na 2011 na kuvuruga tena usalama katika maeneo ya mpakani mwa DRC na Uganda, Rwanda na Burundi, ambako dazeni kadhaa za makundi ya wanamgambo zinaendesha shguhuli zake.

Tshikedi aliwania dhidi ya mgombea alieteuliwa na kabila mwenyewe Emmanuel Ramazani Shadary, na kiongozi mwingine wa upinzani Martin Fayulu, ambaye uchunguzi wa maoni ya wapigakura kabla ya uchaguzi ulimuonyesha akiongoza kinyanganyiro hicho.

Chanzo:DW

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post