YANGA KUFUNGA KAMBI YA MAPINDUZI LEO NA KUPANDA BOTI

Wachezaji wa Yanga.

Klabu ya Yanga inatarajia kucheza mchezo wake wa mwisho wa hatua ya makundi ya Kombe la Mapinduzi 2019, leo Jumatano dhidi ya Jamhuri ya kisiwani Pemba. 

Katika mchezo huo, Yanga itakamilisha ratiba tu na kisha kupanda boti tayari kwa kurejea Jijini Dar es salaam kutokana na kutofuzu hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

Yanga ni ya pili toka mkiani katika kundi A kwa pointi zake tatu, ikishindwa kufanya vizuri katika mechi zake tatu za awali, baada ya kushinda mechi moja pekee na kufungwa mechi mbili.

Katika kundi hilo, Azam inaongoza ikiwa na pointi saba sawa na Malindi ambazo zote zimefuzu hatua ya nusu fainali. Jamhuri ina pointi nne, Yanga ina pointi tatu na KVZ inaburuza mkia na pointi moja.

Michuano hiyo ambayo ilianza Januari Mosi mwaka huu, inazishirikisha timu tisa, tatu za Tanzania Bara na sita za Zanzibar na itahitimishwa Januari 13.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527