SABABU KWANINI JANUARI NDIYO MWEZI WA KWANZA WA MWAKA


Kila mwaka tarahe kama hii watu kutoka kote duniani hukaribisha mwaka mpya kwa fataki, kupiga filimbi, pambaja na vinywaji.

Lakini kabla ya kuanza sherehe hizo je hujafikiria ni kwa nini tarehe mosi Januari ndio inayoadhimisha kuanza kwa mwaka mpya?

Kila kitu kinatokana na mila na tamasha za Roma, na kalenda iliozinduliwa na Julius Caesar miaka 2000 iliopita.

Lakini pia huwezi kumwacha nje papa aliyejulikana kwa jina Gregorio wa kumi na tatu.

Hebu tuone ni kwa nini?

Kwa Waroma wa zamani .Januari ilikuwa muhimu kwa sababu ulikuwa mwezi uliotakaswa kwa mungu Janus (hivyobasi ukaitwa Ianuarius, ikimaanisha Januari kwa kilatino.}"Inahusishwa na kuangalia mbele na nyuma," anaelezea Diana Spencer, profesa katika Chuo Kikuu cha Birmingham nchini Uingereza.

"Kwa hiyo ikiwa kuna muda katika mwaka ambao unapaswa kuamua, huu ndiyo wakati tunapoanza tena." Ni mantiki kuwa hivi ".

Pia unafanana na muda kama ule wa Ulaya ambapo siku zinaanza kuwa ndefu baada ya msimu wa baridi.

"Waroma walihusishwa nao sana kwa sababu hutokea baada ya siku fupi, wakati ambapo dunia ina giza ,baridi na hakuna kitu kinachomea, kulingana na Professa Spencer.

''Ni Muda wa kupumua na kutafakari''.

Baada ya Waroma kuwa na mamlaka zaidi, walianza kusamabaza kalenda yao katika ufalme wao mkubwa.Kulingana na itikadi za Roma, Janus ni mungu wa nyuso mbili, mwanzo na mwisho .

Lakini katika miaka ya kati , baada ya kuanguka kwa ufalme wa Roma , Ukristo uliakuwa umejiimarisha hivyobasi tarehe mosi januari ilionekana kuwa tarehe ya Kipagani.

Mataifa mengi yaliotawaliwa na Ukristo walitaka mwaka mpya kuadhimishwa tarehe 25, ambayo inaadhimisha tarehe ambayo malaika Jibreel alijitokeza kwa bikra Mariam mtakatifu.

''Ijapoikjuwa siku ya krisimasi ni siku ya kuyzaliwa kwa Yesu, tarehe muhimu ni wakati malaika huyo alipomwambia Mariam kwamba atajifungua mwana'', Spence aliambia BBC.

Huo ndio wakati ambapo hadithi ya Yesu ilianza , hivyobasi ilikuwa na maana kuu kutaka mwaka mpya kuanza siku hiyo.HPapa Gregorio wa 13 alishinikiza mwanzo wa mwaka kuwa mwezi Janurai badala ya mwezi Machi.

hatahivyo Uingereza ambayo ilipinga amri ya papa na kuchukua dini ya Wapinzani wa papa waliendelea kusherehekea Machi 25 hadi mwaka 1752.

Mwaka huo sheria ya bunge la Uingereza ilioana ile ya mataifa menbgine ya Ulaya.

Leo, mataifa mengi huongozwa na kalenda hiyo ya Gregorian, na ndio sababu fataki hupigwa kote duniani ifikiapo tarehe mosi mwezi januari kila mwaka.

Katika karne ya kumiIn the sixteenth century, Pope Gregory XIII introduced the Gregorian calendar, and January 1 was restored as a new year in Catholic countries.
Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527