MPIRA WA KOMBE LA DUNIA WASHINDANISHWA NA YAI


Mpira wa Kombe la Dunia 2018 na picha ya yai iliyoweka rekodi.

Shirikisho la soka duniani (FIFA), kupitia ukurasa wake wa 'Instagram' limeanza mchakato wa kuisaka rekodi ya picha iliyopendwa zaidi (Likes) kwenye mtandao huo ili kuvunja rekodi ya picha ya yai.

FIFA wameomba wafuasi wao na wapenzi wa mpira duniani kuipenda picha hiyo ili iweze kuweka rekodi ya pekee katika mtandao huo.

''Mapema leo picha ya yai imeweka rekodi ya kuwa chapisho lililopendwa zaidi na ndipo tukafikiria kuwa picha ya mpira wa kombe la dunia iweze kuweka rekodi ya kupenda zaidi'', amesema.

Picha ya yai iliyopandishwa Januari 4, 2019 mapema leo ikafikisha 'likes' zaidi ya milioni 18 ambazo zilikuwa ndio nyingi zaidi kwa picha ya Kylie Jenner.

Mpaka sasa picha hiyo ya yai imependwa mara milioni 28.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527