WAZIRI MKUU UINGEREZA ASHINDWA KUJITOA UMOJA WA ULAYA 'BREXIT'

Waziri Mkuu wa Uingereza ameshindwa vibaya katika kura ya kujitoa katika Umoja wa Ulaya – maarufu kama Brexit – katika bunge la Uingereza baada ya wabunge kupinga mswaada wake kwa kura 432 kwa 202.

Mara baada ya kipigo hicho, May amesema kuwa kutokana na wingi wa kura za kupinga mswaada huo serikali yake itaruhusu mswaada wa kutokuwa na imani kujadiliwa bungeni.

Aidha, wakati anarudi kukaa chini, kiongozi wa chama cha upinzani cha Leba, Jeremy Corbyn mara moja alithibitisha kuwa amewasilisha kura ya kutokuwa na imani na serikali ya May, mswaada ambao utajadiliwa Jumatano.


Hata hivyo, May alikuwa amewasilisha mbele ya bunge mpango mzima wa jinsi Uingereza itakavyojitoa katika Umoja wa Ulaya suala ambalo liliidhihirishwa katika kura ya maoni mwaka 2016.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post