BOT YAIFUNGA BENKI NYINGINE

Naibu Gavana Dk. Bernad Kibese.

Benki Kuu ya Tanzania BOT imehamishia mali na madeni yote ya Bank M kwenda Azania Bank baada ya benki hiyo kushindwa kuwahudumia wateja wake pamoja na kulipa madeni yao.

Akitangaza taarifa hiyo asubuhi ya leo Januri 14, Naibu Gavana Dk. Bernad Kibese amesema kwamba baada ya kutafuta njia mbalimbali za ufumbuzi wa matatizo ya Benk M, muafaka uliopatikana ni kuhamisha mali zote kwenda Benki ya Azania Bank Limited kwa mujibu wa sheria.

Aidha Dk. Kibese ameeleza kwamba wateja wenye mikopo wametakiwa kuendelea kulipa mikopo yao kulingana na mikataba yao huku benki kuu ikiahidi kufuatilia suala hili kwa ukarubu zaidi.

Aidha Dk Kibese amewatoa wasiwasi wateja wanaohamishiwa Azania Bank, kwamba Benki hiyo inatarajia kuwa na mtaji wa shilingi bilioni 164, ambayo ni kiwango cha juu cha mtaji unatakiwa kuendesha shughuli za kibenki ambayo ni zaidi ya shilingi bilioni 15 hivyo itaweza kuhudumia wateja wake wa zamani na wapya.

Benki kuu itaendelea kulinda maslahi ya wateja wa huduma za kibenki na kuimarisha uhimilivu wa sekta ya fedha nchini.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527