KINA MAMA NA WATOTO WAJITOLEA KUIMARISHA ULINZI MITAANI

Wanawake wanaoishi maeneo ya mabanda nchini Kenya wamejitolea kukabiliana na ukosefu wa usalama katika maeneo yao, jukumu ambalo kwa muda mrefu liliachiwa wanaume.

Wanawake wanaoishi maeneo ya mabanda nchini Kenya wamejitolea kukabiliana na ukosefu wa usalama katika maeneo yao, jukumu ambalo kwa muda mrefu liliachiwa wanaume.

 Kupitia mpango walioupa jina ‘wamama na usalama' wanawake hao wanasema wanatambua jukumu lao kubwa la kuielekeza jamii ndiposa wanataka kuwa mstari wa mbele katika harakati za kukabiliana na ukosefu wa usalama. 

Maeneo ya mabanda yanasifika kwa kila aina ya uhalifu hali inayochangiwa na wingi wa watu, umasikini na kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira.

 Kina mama na watoto huathirika zaidi kutokana na visa vya uhalifu katika maeneo hayo huku vijana wakilaumiwa zaidi kwa kusababisha uhalifu.

Chanzo:Dw

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527