NAHODHA WA SIMBA ATOA SIRI ZA AUSSEMS KWA WAARABU

Nahodha wa klabu ya soka ya Simba, John Bocco amesema kocha Patrick Aussems anatumia michuano ya mapinduzi kwa kutengeneza ushindani kwa kila mchezaji kwaajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya JS Souara.

Bocco ameysema hayo akiwa visiwani Zanzibar ambako Simba inashiriki michuano hiyo ambayo imeshuhudiwa kocha Patrick Aussems akibadilisha wachezaji wake katika mechi mbili ambazo tayari ameshacheza.

''Haya mabadiliko anayoyafanya kocha ni kuelekea mechi yetu ya kimataifa, kila mchezaji anatakiwa kuwa imara na tayari kwa mchezo maana timu nyingine inaweza kubaki huku Zanzibar wengine wakaenda kucheza mchezo wetu wa Jumamosi dhidi ya JS Souara'', amesema Bocco.

Katika michuano ya Mapinduzi Simba ilishinda mchezo wake wa kwanza kwa mabao 4-1 dhidi ya Chipukizi ya Zanzibar kabla ya jana usiku kuifunga KMKM kwa bao 1-0.

Kwa mujibu wa ratiba ya kikosi hicho endapo kitafuzu nusu fainali ya Mapinduzi Cup watabaki wachezaji wa kikosi cha pili huku wale wa kikosi cha kwanza wakirejea Dar es salaam tayari kwa mchezo wao wa kwanza hatua ya makundi.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527