WHOZU AFUNGA MWAKA NA NDINGA JIPYA,ASEMA MATUNDA YA TIGO FIESTA

Mchekeshaji na mburudishaji chipukizi hapa Tanzania, Whozu amefanikiwa kutimiza ndoto yake ya kumiliki gari, hii ni baada ya kupata nafasi ya kutumbuiza kwenye mikoa 13 kwenye tamasha la Togo Fiesta.

Whozu ameshea na mashabiki wake picha ya gari hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kuandika “Wengi walikuwa wananitizama kama mchekeshaji lakini clouds wakanitizama kama entertainer…wakanifungulia dunia nakunipa Nafasi ya mimi kujifungulia maisha…. Kuperfom Fiesta 13 kati ya Fiesta 15 Mungu ni mwema #mynewride mpiraaa mpyaaaa napiga round nazunguka dar nzima nikimaliza naunganisha kwenda moshi..MUSIC PAYS #MatundaYaTigofiesta“

Kwa upande mwingine, Whozu amewashukuru pia mashabiki wake, vyombo vya habari na Maproducer waliomsaidia kwa kuandika “Niwashukuru pia Mshabiki zangu Asanteni sana kwa support Mwenyezi Mungu Awabariki sana.Shukrani pia Kwa Media Zote Nawashukuru kwa Nafasi yangu Kwenu🙏 Shukrani pia kwa Producers @osam_lucifer Hakika najua unafuraha Uliniamini Nami nikakuaminisha. Pia Zombie Langu @s2kizzy haha Nilikwambia Lakini! Asante pia Directors @lucca_swahili & @joowzeytz May God bless you all Fam & Fans“.

Whozu mwaka huu (2018) amefanya vizuri kwenye muziki na ngoma yake ya Huendi kwa Mbinguni, na ndio wimbo uliomfanya atumbuize karibia mikoa yote iliyopitiwa na Fiesta.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527