IDADI YA VIFO KUTOKANA NA KIMBUNGA CHA TSUNAMI YAONGEZEKA INDONESIA

Idadi ya vifo iliyotokana na janga la kimbunga cha Tsunami kilichoikumba Indonesia inaendelea kuongezeka. Watu 373 wamethibitishwa kupoteza maisha na wengine 1,400 wamepata majeraha.
Kwa mujibu wa DW Swahili, Idadi hiyo ya vifo inategemewa kuongezeka zaidi, huku watu 128 wakiwa hawajulikani walipo hadi sasa hasa katika maeneo yaliyoathirika vibaya ya pwani ya kisiwa cha magharibi cha Java na kisiwa cha kusini cha Sumatra.

Juhudi za kutafuta miili ya mamia ya watu pamoja na kuwanusuru waliopata majeraha zimeongezeka leo hii kufuatia kimbuga cha Tsunami cha hivi karibuni kilichopiga nchini Indonesia. Wataalamu wamekusanya ushahidi unaothibitisha kwamba kimbunga hicho kilichochewa na mlipuko wa volkano.

Ni kwa mara ya pili kimbunga cha Tsunami kinapiga Indonesia ndani ya mwaka huu. Matetemeko makubwa ya ardhi yalichochea kimbunga hicho cha Tsunami na kupiga kisiwa cha Sulawesi mwezi Septemba.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527