TETESI ZA SOKA JUMAPILI DEC, 30 2018

Christian Pulisic
Chelsea wametoa ofa ya hadi pauni milioni 45 kumsaini mshambuliaji wa Borussia Dortmund Christian Pulisic msimu ujao lakini klabu hiyo ya Ujerumani itacheleweza uamuzi wake inaposubiri ofa kutoka kwa vilabu vingine kwa mchezaji huyo raia wa Marekani mwenye miaka 20. (ESPN)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez anataka kumwendea straika wa Leeds Kemar Roofe, 25, ikiwa atapewa pesa mwezi Januari. (Sunday Mirror)

Meneja wa muda wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer amewashauri kipa wa Uhispania David de Gea, 28, na mshabuliaji Mfaransa Anthony Martial, 23, kusaini mikataba mipya na klabu hiyo. (Mail on Sunday)David de Gea
Chelsea wameambiwa kuwa ni lazma walipe pauni milioni 30 ikiwa wanataka beki mjerumani Mats Hummels, 30, mwezi Januari. (Sun on Sunday)

Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri amekana madai kuwa anataka kuwa meneja mpya wa msimu ujao. (Mail on Sunday)

Meneja wa Watford Javi Gracia anasema sio jambo la kushangaza kuwa Abdoulaye Doucoure, 25 anahusishwa na kuhama licha ya yeye kutarajia raia huyo wa Ufransa kuendelea kubaki kwa muda zaidi. (Independent)Nathaniel Clyne
Cardiff wanaongoza mbio za kumwinda beki wa Liverpool Nathaniel Clyne, licha ya Fulham na Leicester nao kuwa na nia ya kumsaini kiungo huyo wa miaka 27 raia wa England. (Sunday Mirror)

Mlinzi wa Manchester United raia wa Italia Matteo Darmian, 29, analengwa na Inter Milan na Lazio. (Calciomercato)

Lazio watajia kuwasaini mlinzi wa Chelsea raia wa Italia Davide Zappacosta, 26 ikiwa Manchester United watakataa kumuuza Darmian. (Sunday Mirror)

Arsenal wamejiunga na mahasimu wao Tottenham kutaka kumsiani beki wa Norwich City mwennye miaka 18 Max Aarons. (Sunday Mirror)Davide Zappacosta

Liverpool wanammezea mate kiungo wa kati wa Trabzonspor Abdulkadir Omur, 19, lakini wanakabaliwa na ushindani kutoka Manchester City and Roma. (Fotomac, via Star on Sunday)

Meneja wa Southampton Ralph Hasenhuttl anataka kumiania beki wa Olympiakos na Norway Omar Elabdellaoui, 27, mwezi Januari. (Mail on Sunday)

Beki wa Leicester City raia wa Australia Callum Elder, 23, anajifunza na Ipswich Town na anatarajiwa kujiunga kwa mkopo mwezi Januari. (East Anglian Daily Times)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527