TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU DEC 24 2018, JUVENTUS WAMWINDA LUKAKU

Juventus imeonyesha kutaka kumsajili mshambulaji wa Manchester United Mbelgiji Romelu Lukaku ,25, (Calciomercato-in Rome)

Timu ya Juventus ya Italia inataka kumsajili kiungo wa Arsenal na timu ya Taifa ya Wales Aaron Ramsey, 27, akiwa mchezaji huru (sky Italia)

Lakini pia nayo timu ya Buyern Munich ya Ujeruman bado inavutiwa na mchezaji huyo wa zamani wa Cardiff(Mail)Aaron Ramsey

Arsenal inaweza kuvunja rekodi yake ya usajili kwa kutaka kumsajili mchezaji wa Lille ya Ufaransa Nicolas Pepe na timu yake hiyo itaka dau la pauni Milioni 72 ili kumuuza winger huyo wa Ivory Coast. (Telefoot,via Metro)

Mchezaji wa zamani wa Chelsea Tony Cascarino ameitaka timu yake hiyo ya zamani kumsajili mshambuliaji wa West Ham United Marko Arnautovic (Talksport)

Timu ya Lazio ya Italia inamtaka mshambuliaji wa timu ya Southampton Manolo Gabbiadini ,27, (La Nazione - In Italia)

Fulham inataka kumsajili mlinzi wa kati wa timu ya Besiktas ya Uturuki Domagol Vida raia wa Croatia (Fotomac - Uturuki)

Kocha wa Newcastle Rafael Benitez anatamani kusajili winga mwezi ujao ukufunguliwa usajili wa dirisha dogo (Chronicle)

Winger wa Bayern Munich Mfaransa Frank Ribery amewwka milango wazi wa timu yake hiyo kumuongezea mkataba kwa msimu ujao (Sky,via Goal)

Mashabiki wa timu ya Birmigham City wamesikirishwa na kitendo cha timu yao kukosa tiketi za ziada kwaajili ya mchezo wa kombe la FA dhidi ya West Ham utakaochezwa January 5 (Birmingham Mail).

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527