Breaking : RAIS MAGUFULI AFUTA KIKOKOTOO KIPYA CHA MAFAO..AONDOA STRESS ZA WASTAAFU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amegiza vikokotoo vya mafao ya wafanyakazi katika mifuko ya hifadhi ya jamii vilivyokuwa vinatumika kabla ya mifuko ya kuunganisha viendelee kutumika kwa kila mfuko hadi mwaka 2023. 

Rais Magufuli ametoa uamuzi huo leo tarehe 28 Desemba 2018 alipokutana viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini, watendaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii na mawaziri wa wizara husika, kwa ajili ya kujadili masuala yahusuyo mafao ya wafanyakazi ikiwemo kuhusu kanuni mpya ya kukokotoa mafao ya wastaafu.

Tazama hapo chini nukuu ya maneno yote aliyoyasema leo 

1. Nimewasikiliza, kimsingi lina umuhimu, na ndio maana nimeona niwaite, na hasa kwa sababu nimekuwa nikisikiliza maelezo hata ya regulator, yanakuwa too academic. 

2.Ukishatoa maelezo ambayo ni too academic, unaelezea wastaafu, na kustaafu ni sifa na heshima, ulifanya kazi yako kwa uadilifu mkubwa, umesacrafice maisha yako kwa ajili ya kazi. 

3. Unapoona hiyo heshima inakuwa karaha, mateso, inafrustrate kwa mfanyakazi yoyote, sasa mimi siko hapa kumfrustrate mtu, kwani hata mimi nilikuwa mfanyakazi. 

4.Tuliamua kuunganisha mifuko, tulikubaliana NSSF ufanyiwe marekebisho, hatua hii ilitokana na ombi la muda mrefu la vyama vya wafanyakazi waliotaka hii mifuko iunganishwe. 

5.Mifuko ya jamii yote ilikuwa na hali mbaya, kwa sababu haikuwa coordinated, waendesha mifuko wote walikuwa wanapigana vita, wanagombania wanachama, walikuwa hawapendani. 

6.Mingine ilikuwa ikiendeshwa kiajabu, pakawa panaanzishwa miradi ya kiajabu, na miradi mingi ilikuwa ya majengo, nenda Kigamboni kaangalie yale majengo ya ndege vilaje, its a huge thing'. 

7.Tulipongia madarakani tulikuta deni trilion 1.2, serikali yenyewe haijachangia hii mifuko, waliostaafu kwa wakati ule ilikuwa ni shida, kwani hata ile michango ya serikali haitekelezwi. 

8.Tukaanza kulipa madeni, mpaka mwezi Machi mwaka huu madeni yote yalikuwa yamemalizika kulipwa. 

9.Matatizo yapo lazima tuende kwenye solution, kile kikokotoo angalau imefika 50%, lakini pia hata hawa walioko chini ilifaa ipande, hata hiyo formula inachanganya zaidi.


10.Mishahara mingi ya wafanyakzi serikalini si mizuri, anapofika mwisho unampa kidogo kidogo haingii, si unipe tu yote nikafie mbali, nilipokuwa nachangia hukuniambia, leo nachukua unaniambia nachukua kidogo, hata logic haingii. 

11.hata hawa Mawaziri, wabunge wanachukua hela yao yote, halafu uwaambie utachukua kidogo kidogo kila ukija, hawatakubali, kwenye reality, hata mimi hainingii. 


12.Tunahitaji watu wetu wapate fedha nyingi walipwe, lakini pia tunahitaji huu mfuko usife, hii formula haipo duniani, mtu anamaliza halafu kiwango chake unakizidisha mara 4, haipo.

13. Walioweka formula hii ni makatibu wakuu wa wakati ule, wa wakati wangu hawawezi, kwa sababu kwenye ile mifuko wengine ni beneficiary, ni kosa walifanya. 

14. Hifadhi za jamii zipunguze matumizi ya hovyo, kama mtu anastahili kulipwa 60% hatuwezi kumlipa kwa sababu hifadhi zinafanya matumizi ya hovyo. 

15. Kwa mfano kuna mfuko mmoja unachapisha kalenda kwa 1.3 bilion, hiyo hiyo imeajiri walinzi ambao ni very expensive, wanawalipa bilioni 2 kwa mwaka, wakati wangeajiri SUMA JKT wangewalipa chini ya bilioni 1 kwa mwaka. 

16. Uwekezaji kama ule wa Dege Heko village haufai, ukatumia fedha za wanachama bila ridhaa zao, halafu leo wastaafu uwaambie hamna hela formula imekataa. 

17. Mifuko muweke utaratibu mzuri, ni suala ambalo haliingii akilini nikasubiri mpaka nitakapofika miaka 60 ndio nipate mafao yangu, nimetoa michango yangu, kwanza hayupo atakaye nikumbuka kama nilifanya kazi, hata contructor atakuwa kashakwenda kwao. 

18. Kustaafu sio dhambi, kustaafu ni heshima, lazima awe respected, mwalimu amefundisha ameharibu na macho kutokana na chaki, halafu umpe condition. 

19.Mazungumzo yenu yote nimeyasikia, mimi nimeamua, angalau tuwe na kipindi cha mpito, kikokotoo kilichokuwa kinatumika kwa kila mfuko kabla ya mifuko kuunganishwa, tuendelee katika kipindi cha miaka ya mpito. 

20. Mtu anayestaafu anatakiwa kuheshimiwa, amelitumia taifa hili, amesacrafice, ni shujaa, kustaafu bila kufukuzwa ni heshima, hatakiwi kupata shida, nimeamua kikokotoo kiendelee katika kipindi hiki cha mpito, ambapo ni hadi mwaka 2023. 

21. Mifuko hiyo itakuwa imetengamaa, ni matumaini yangu, nitaichungulia kweli kweli hiyo mifuko, na Waziri natoa maagizo yake, wachungulie kweli, ili kusudi watu wasitumie hovyo hovyo, hii ni mifuko ya wanachama. 

22.Formula nzuri ni zile zinazo wapromote wafanyakazi, ndio ninazozitaka mimi, formula zinazowanyima haki wafanyakazi sio formula nzuri, ninashukuru katika kipindi hiki kifupi cha kuunganisha mifuko tumeanza kuona matokeo.

Vyama vilivyokutana na kuzungumza na Rais Magufuli ikulu jijini Dar es Salaam, ni pamoja na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania(TUCTA), vyama shiriki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (PSSD na NSSF) na Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii (SSRA).

Kanuni mpya ya kikokotoo iliyotolewa hivi karibuni na serikali, ambayo inaelekeza wastaafu kulipwa mkupuo wa asilimia 25 ya mafao pindi watakapostaafu na asimilia 75 inayobaki watakuwa wakilipwa kama pensheni ya kila mwezi.

Baada ya kikokotoo hicho kutangazwa kwa umma, baadhi ya vyama vya wafanyakazi ikiwemo TUCTA, viliipinga kanuni hiyo kwa maelezo kwamba inakandamiza wafanyakazi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527