AJIFUNGUA MTOTO BAADA YA KUPANDIKIZWA UZAZI WA MAMA YAKE

Meenakshi Valand ni mwananamke wa 12 duniani kujifungua mtoto baada ya kupandikizwa mfuko wa uzazi

Meenakshi Valand ni mmoja kati ya watu wachache duniani ambao wamejaaliwa kupata watoto baada ya kupandikizwa mfuko wa uzazi.


"Sikuweza kujizuia kulia baada ya kusikia sauti ya mwanangu akilia. Haya ni machozi ya furaha - Nimepoteza watoto sita katika kipindi cha miaka kadhaa iliyopita," alisema Meenakshi.


Mama huyo wa miaka 28-alijifungua mwezi uliyopita nchini India baada ya kupandikizwa mfuko wa uzazi wa mamake mzazi.

Katika miaka tisa ya ndoa yake, Meenakshi alizaa watoto wawili waliofariki, alipoteza wengine wanne katika uja uzito, hatua iliyomsababisha kukatika kwa mfuko wake wa uzazi.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527