BITEKO ATOA MAAMUZI KILIO CHA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU WILAYANI KAHAMA

Serikali imesikia kilio cha muda mrefu cha wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo ya Bushimangila yaliyopo Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga kwa kutoa idhini kwa wachimbaji hao kuendelea na shughuli za uchimbaji katika machimbo hayo. 

Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko alitoa idhini hiyo jana baada ya kufanya ziara katika machimbo hayo ya Bushimangila kwa lengo la kukagua shughuli za uchimbaji, kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji wadogo wa dhahabu. 

Awali baadhi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu katika machimbo hayo walieleza kufukuzwa na Menan Sanga ambaye anamiliki leseni ya uchimbaji na kuomba serikali kuwapatia leseni ya uchimbaji katika eneo hilo. 

Walisema awali eneo hilo lilikuwa likimilikiwa na kampuni ya utafiti ya Lion Town tangu mwaka 1989 na baadaye likakabidhiwa kwa kampuni ya Chela Resources na sasa Menan Sanga na kwamba limekuwa likibadilishwa umiliki kwa muda mrefu bila kuendelezwa huku wao wakitaabika. 

Na George Binagi-GB Pazzo 
Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Doto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Machimbo ya Bushimbangila wilayani Kahama, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mhandu.
Mbung wa Jimbo la Msalala, Mhe. Ezekiel Maige akizungumza kwenye mkutano huo na kuelekeza kilio cha wachimbaji wa dhahabu katika machimbo ya Bushimangila.
Tazama Video hapa chini




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527