RAIS MAGUFULI KASEMA KOROSHO ZOTE ZITANUNULIWA NA SERIKALI KWA SH 3,300....KAGOMA KUYARUHUSU MAKAMPUNI YANUNUE

Rais Dkt. John Pombe Magufuli amegoma kuyauzia makampuni Korosho kwa madai kwamba ni wababaishaji na wanataka kuwaibia wananchi.


Badala yake amesema kwamba serikali itanunua korosho yote kwa bei ya shilingi 3,300 kwa kilo.


Awali, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kwamba kuna makampuni 13 yamejitokeza kutaka kununua korosho kwa bei elekezi ya tsh. 3000

Aliyataja makampuni hayo kuwa ni Mega movers ambayo inataka tani laki 2, kampuni ya Kitanzania Mkeme Agri inataka tani elfu 5, na makampuni matatu yatachukua tani elfu 5, makampuni manne, tani elfu moja moja. 

Ombi hilo limekataliwa na Rais Magufuli kwa madai kwamba wafanyabiashara hao ni wababaishaji, hivyo korosho yote itanunuliwa na serikali kwa sh 3,300 kwa kilo isiyobanguliwa.

“Hawa wanaokuja leo hawa ni ujajnja tuu kwanini hawakuja mwezi uliopita? watakuja Na macondition ya ajabu. Sisi hatuwezi kukaa kimya wakulima wetu wananyanyaswa. TANTrade muanze kutafuta masoko ya mazao mengine kama cocoa Na mengine”. Amesema Rais Magufuli

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527