WALIMU WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA WIZI WA MITIHANI YA DARASA LA SABA

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Hazina iliyopo Magomeni, Dar es salaam, Patrick Cheche (43) na walimu wenzake wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwa ni pamoja na kupata mitihani na kutoa maudhui ya mitihani hiyo kwa watahiniwa wa darasa la saba isivyo halali.

Akiwasomea hati ya mashtaka leo Septemba 26, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono aliwataja washtakiwa hao kuwa ni mwalimu Laurence Ochien (30), mkazi wa Magomeni Makuti.

Wengine ni mwalimu Justus James (32) Mkazi wa Kimara Mwisho Mavurunza, Nasri Mohammed (32) Mkazi wa Magomeni Makuti.



Na Tausi Ally,Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527