KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, ALA KIAPO CHA UJUMBE TUME YA UTUMISHI, JESHI LA POLISI, MAGEREZA NA UHAMIAJI


Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akila kiapo cha uadilifu mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Dkt. Eliezer Feleshi kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi kwa Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, pamoja na Uhamiaji. Kiapo hicho kilifanyika katika Ofisi za Mahaka Kuu ya Tanzania, leo Septemba 4, 2018 jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama akila kiapo cha uadilifu mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Dkt. Eliezer Feleshi kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi kwa Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, pamoja na Uhamiaji.
Jaji Kiongozi, Dkt. Eliezer Feleshi wa Mahakama Kuu ya Tanzania (meza kuu) akifanya mazunguzo na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(kulia) baada ya kula kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi kwa Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza na Uhamiaji.
Jaji Kiongozi, Dkt. Eliezer Feleshi wa Mahakama Kuu ya Tanzania(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(kushoto) mara baada ya kula kiapo cha kuwa Mjumbe wa Tume ya Utumishi kwa Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza na Uhamiaji. Kulia ni Kamishna wa Jeshi la Magereza, Uwesu Ngarama. (Picha na Jeshi la Magereza).

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527