GUMZO LA DIAMOND KUTAKA KUROGWA : SHILOLE NAYE AMCHANA

Bado kile kinachodaiwa kuwa Hamisa Mobetto alitaka kumroga Diamond Platnumz na familia yake kinazidi kuchukua nafasi kwenye mitandao ya kijami.

Mjadala umekuwa mpana hasa kwa kauli aliyoitoa jana Diamond kupitia Wasafi TV ingawa upande wa Hamisa amekuwa kimya kwenye suala hilo.

Sasa muimbaji Shilole hajawa nyuma kwenye hilo ameposti picha ya Diamond Platnumz (ipo chini) na kuisindikizia na caption iliyosema;'Ndio maana wanakuroga, medamshi sana kaka yangu Diamond Platnumz,'.
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amezaa mtoto mmoja na Diamond Platnumz na utakumbuka hadi muimbaji huyo anakiri kuwa amezaa na Hamisa ilikuwa ni baada ya mvutano mrefu na hii ni kutokana kipindi hicho Diamond bado alikuwa na mahusiano na Zari.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527