WANACHAMA WA CCM WAANDAMANA KUMKATAA MBUNGE ALIYETOKA CHADEMA

Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli wameandamana kwenye ofisi za chama hicho wakitaka aliyekuwa Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Julius Kalanga aliyejiunga na chama hicho kufuata utaratibu ikiwemo hatua za uteuzi wa nafasi ya kugombania ubunge.


Aidha, Wakizungumza katika Ofisi hizo wamesema kuwa wamesikia taarifa za kuteuliwa kwake bila kufuata utaratibu ikiwemo kukaa vikao na wazee wa kimila Malaigwanani ili waweze kumpitisha.


Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Monduli amesema kuwa hajashiriki kwenye vikao na wazee wa kimila kama inavyodaiwa na baadhi ya wanachama hao na kwamba utaratibu utatumika katika kuwapata wagombea


“Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinataratibu zake, kina katiba, sheria ambazo zote zitafuatwa katika mchakato huu wa kumpata mgombea ubunge wa jimbo hili la Monduli,”amesema mwenyekiti wa chama wilaya ya Monduli, Wilson Lengima

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527