RAIS MAGUFULI ATEUA MAJAJI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali na Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.

Kabla ya uteuzi huo Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali alikuwa Jaji Kiongozi na Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Uteuzi huu umeanza jana Juni mosi, 2018.

Aidha, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imesema tarehe ya kuapishwa kwa Majaji hao itatangazwa hapo baadaye.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527