TATU MZUKA YATANGAZA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA NA WEMA SEPETU


Bi Wema Sepetu akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)  kuhusu Kampuni ya ‘The Network’ ambayo ni kampuni mama inayoendesha  mchezo wa namba wa Tatu Mzuka nchini Tanzania, kutangaza kuanza  ushirikiano nae wa kibiashara. 
Wema Sepetu akifurahia jambo mara baada ya kutangazwa ushirikiano wake na kampuni ya The Netwek-ambayo ni kampuni mama inayoendesha mchezo wa namba wa Tatu Mzuka nchini Tanzania
Kampuni ya ‘The Network’ ambayo ni kampuni mama inayoendesha mchezo wa namba wa Tatu Mzuka nchini Tanzania, jana imetangaza kuanza ushirikiano wa kibiashara na mrembo maarufu nchini Bi. Wema Sepetu.

Ushirikiano huu ni mwendelezo wa mpango mkakakati wa Tatu Mzuka wa kufanya kazi bega kwa bega na Watanzania katika kuboresha maisha yao. Kusudi hasa la Tatu Mzuka kama ilivyoelezwa ni kusambaza fursa kwa watu wengi kadri inavyowezekana ili kubadilisha maisha yao.

Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Bwana Sebastian Maganga alisema kwamba ushirikiano huu ni mmojawapo kati ya nyingi ambazo Tatu Mzuka wanajihusisha nazo.‘Muda wote tunaangalia kipaji ambacho tunahisi kinaendana na bidhaa yetu na hivyo kuanzisha ushirikiano wa kibiashara. Katika biashara yetu tayari tuna ushirikiano na Millard Ayo, Brother K, Shilawadu na wengine wengi na leo tunatangaza kumwongeza Wema Sepetu kwenye orodha hiyo’ alisema Maganga.

Wema ambaye alikuwepo pia kuelezea furaha yake baada ya kutangaza ushirikiano na Tatu Mzuka, alisisitiza kwamba ana hamu kubwa ya kuanza kuwashirikisha mashabiki wake mambo mazuri ambayo amewaandalia.‘Ninawashukuru sana Tatu Mzuka kwa ushirikiano huu, ambao hakika sio tu utanigusa mimi bali mashabiki zangu na watanzania kwa ujumla wao katika kujitengenezea fursa za kuboresha maisha yao’ alisema Wema.

Wema alisema kwa kuanza, anaomba mashabiki zake wachangamkie fursa ya kucheza Tatu Mzuka, ambapo kama unatumia MPESA, TIGO PESA au AIRTEL MONEY, unaingiza namba ya kampuni ambayo ni 555111 na baada ya hapo unaweka namba zako 3 za bahati zikifuatiwa na jina langu WEMA na baada ya hapo ingiza kiasi unachotaka kuanzia shilingi 500 mpaka 30,000. 

‘Pamoja na kujiongezea nafasi za kushinda za kawaida za Tatu Mzuka kila saa hadi milioni 6, kila siku unaweza kushinda milioni 10 pamoja na zaidi ya milioni 140 kila Jumapili, utapata fursa zaidi ya zawadi mbalimbali kutoka kwa Wema’ alisema Wema. Pamoja na utambulisho wa Wema, Tatu Mzuka pia ilitangaza kwamba Jumapili hii ya tarehe 13 ambayo ni siku ya mama duniani kuna milioni 140 ambayo lazima itolewe kwa mtu mmoja pamoja na mama yake.

‘Hii ni fursa kwa kila mtanzania ambaye kwa namna moja ama nyingine angependa kumshukuru mama yake au mlezi wake kwa kazi kubwa aliyofanya, na hivyo ukicheza sasa, unaingia kwenye Mzuka Deile ambayo inafanyika kila siku Jumatatu hadi Jumamosi, ambapo milioni 10 lazima itoke kwa mtanzania mmoja na yeye atamgawia mama yake milioni 3, wakati Jumapili hii kwenye Mzuka Jackpot yeyote atakayeshinda milioni 140 atambusti mama yake kwa milioni 30’ alihitimisha Maganga
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Bwana Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Waandishi wa habari mapema jana jijini Dar kuhusu Kampuni ya ‘The Network’ ambayo ni kampuni mama inayoendesha mchezo wa namba wa Tatu Mzuka nchini Tanzania, kutangaza kuanza ushirikiano wa kibiashara na mrembo maarufu nchini Bi. Wema Sepetu pichani kushoto. 

‘Muda wote tunaangalia kipaji ambacho tunahisi kinaendana na bidhaa yetu na hivyo kuanzisha ushirikiano wa kibiashara. Katika biashara yetu tayari tuna ushirikiano na Millard Ayo, Brother K, Shilawadu na wengine wengi na leo tunatangaza kumwongeza Wema Sepetu kwenye orodha hiyo’ alisema Maganga. 

Wema ambaye alikuwepo pia kuelezea furaha yake baada ya kutangaza ushirikiano na Tatu Mzuka, alisisitiza kwamba ana hamu kubwa ya kuanza kuwashirikisha mashabiki wake mambo mazuri ambayo amewaandalia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527