POLISI YAWAFUNGULIA JALADA LA WATU WANAOSAMBAZA PICHA ZA VITABU MTANDAONI

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amesema jalada la uchunguzi wa watu wanaosambaza vitabu mitandaoni limefunguliwa.

Akizungumza jana Ijumaa Mei 4, 2018 katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Kamanda Sirro amesema wamepokea maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.


"Tumepokea maelekezo na tayari tumefungua jalada na tutakapowapata tutawapeleka mahakamani," alisema IGP Sirro.


Kuhusu watu wanaovunja sheria ya mitandao, IGP Sirro amesema wanaendelea kufuatilia na kila atakayekuwa anabainika wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527