Mchekeshaji maarufu bongo Ebitoke amesema ndoto anayoiota ya kuja kukanyaga ardhi ya Hollywood siku moja, ana imani itatimia na iwapo atakufa bila kutimia basi atakufa bila kuwa na amani.
Akiwa KIKAANGONI East Africa Television, Ebitoke amesema kwamba ndoto yake kubwa siku moja ni kuigiza filamu za Hollywood na kufanya kazi na wasanii wa Hollywood, na hata watu wakitaja Hollywood wawe wanaitaja na Tanzania.
Ndoto yangu ni kufika Hollywood, nikifa bila kutimiza hiyo ndoto, sidhani kama nitaenda kwa amani, nataka watu watakapotaja Hollywood waitaje na Tanzania, Mimi nataka niwe hata zaidi ya Lupita Nyong'o, yaani nikilala nikiamka naiota Oscar hii hapa, na mpaka niipate”, amesema Ebitoke
Ebitoke ameendelea kwa kusema kwamba hata filamu yake ambayo ameigiza akisubiri kuitoa ina viwango vya kimataifa, na wana malengo ya kuiingiza kwenye tuzo za kimtaifa ili iweze kufika Hollywood.