POLISI ANAYEDAIWA KUUA MDOGO WAKE HECHE AFIKISHWA MAHAKAMANI

Askari polisi E. 1156 William Marwa amefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu mkazi wilaya ya Tarime, akikabiliwa na shtaka la mauaji ya Saguta Chacha ambaye ni mdogo wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.


Mshtakiwa huyo amesomewa kesi ya mauaji namba, PI 76/2018 mbele ya Hakimu A.R. Kahimba leo Aprili 30.


Askari huyo anayedaiwa kutenda kosa hilo Aprili 27 hakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527