MPENZI WA MASOGANGE ATOBOA SIRI

Msanii wa filamu bongo Rammy Galis ambaye alishawahi kuwa kwenye mahusiano na Agnes Masogange aliyefariki hapo jana, ametoa siri ambayo wengi walikuwa hawaijui kuhusu maisha ya Agnes.


Kwenye ukurasa wake wa instagram Rammy Galis ameandika ujumbe akionesha kuhuzunishwa na kifo cha mrembo huyo ambaye alibarikiwa na Muumba kwa urembo wake, na kusema kwamba walipokuwa kwenye mahusiano aliwahi kucheza filamu yake ambayo kama ilitabiri kifo chake, kwa kuigiza kufa mwisho wa kisa hiko kilichopewa jina la 'hukumu'.


“Tulikesha usiku na mchana ili ucheze filamu yetu kwa hisia, ukasema hii iwe kumbukumbu yako kama niliwahii hata kwenye kazi zako kukusaidia, sasa kwanini filamu yetu tulitunga jina liitwe #hukumu? ilikuwaje story ya filamu mwisho unafariki? kwani tulikua tunatungia iwe kweli hukumu yako? Mungu ndio hakimu wa viumbe vyote katika dunia , umeondoka ghafla sanaa , na hii pia ni funzo umeniachia”, ameandika Rammy Galis akiambatanisha picha ya wawili hao pamoja.


Kutokana na kauli hii ya Rammy Galis, tunaweza sema Masogange naye amepitia kifo ambacho muigizaji nguli wa filamu za bongo Steven Kanumba alifariki, kwa kuigiza kifo kwenye filamu yake ya mwisho, na kweli kabla ya filamu kutoka alipatwa na mauti.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527