TUME YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJINA 27 YA WAGOMBEA UDIWANI




Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa majina 27 ya wagombea udiwani walioteuliwa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kuwania nafasi hizo katika kata 10.


Uchaguzi mdogo katika kata hizo utafanyika Februari 17,2018 kutokana na baadhi ya madiwani kujiuzulu nyadhifa zao na vifo.


Katika uteuzi huo wanaume waliojitokeza kugombea nafasi hizo ni 24 na wanawake ni watatu.


Taarifa iliyotolewa na NEC leo Ijumaa Januari 26,2018 imesema wagombea wa kata nne waliteuliwa Januari 20 na wengine wa kata sita waliteuliwa Januari 24,2018.


Wagombea waliojitokeza kuwania udiwani katika kata ya Buhangaza iliyoko wilayani Muleba mkoani Kagera na vyama vyao ni Jenitha Tibihenda (CCM), Nelson Makoti (Chadema) na Grayson Aniceth (NCCR Mageuzi).


Katika Halmashauri ya Siha iliyoko mkoani Kilimanjaro ambako kuna kata tatu zitakazofanya uchaguzi mdogo, wagombea katika kata ya Gararagua ni Zakaria Lukumai (CCM) na Agness Lasway (Chadema). Kata ya Donyomuruak wagombea ni Lwite Ndossi (CCM) na Daniel Molle (Chadema), wakati katika kata ya Kashashi wagombea ni Suzan Natai (CCM) na Immanuel Saro (Chadema).


Mkoani Mwanza ambako kuna kata mbili, wagombea wa kata ya Kanbyelele iliyoko Halmashauri ya Misungwi ni Marco Yela (ACT Wazalendo), Daniel Makoye (CCM) na George Mhoja (Chadema). Kata ya Isamilo iliyoko wilayani Nyamagana wagombea ni Nyamasiriri Marwa (CCM), John Kisyeri (Chadema), Hashim Ramadhan (CUF), Georgina Kibendegele (DP) na Ramadhani Mtoro (UDP).


Kwenye kata ya Mitunguruni iliyoko wilayani Singida wagombea ni Abdallah Mkoko (CCM), Manase Kijanga (Chadema) na Abdallah Kinga (CUF).


Wagombea wa Kata ya Madanga iliyoko wilayani Pangani mkoani Tanga ni Mohamed Abdallah (ACT Wazalendo), Athuman Tunutu (CCM) na Swaibu Mwanyoka (CUF).


Mkoani Dodoma ambako pia kata mbili zitafanya uchaguzi, kata ya Manzase iliyoko wilayani Chamwino wagombea ni Amos Mloha (CCM), Alex Chalo (Chadema) na Ndahani Mazengo (Chaumma), wakati kata ya Kimagai wilayani Mpwapwa mgombea ni Noah Lemto aliyepita bila kupingwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527