MCHUNGAJI MSIGWA ADAI KUNA NJAMA ZA KUMWANGAMIZA

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Chadema Mchungaji Peter Msigwa amesema mbinu inayotumika kuwashawishi na kuwanunua madiwani wa Chama hicho imelenga kupunguza nguvu zake katika kuikosoa Serikali.


Amesema taarifa hizo amepewa na viongozi wa CCM ambao wamemthibitishia kuwa hawana shida nao.


"CCM hawana shida na madiwani, wanachama wanashida na wale wakosoaji wakubwa wa Serikali Kuu"amesema Msigwa


Msigwa amewataja wabunge wengine wa upinzani aliodai watapitia kipindi hicho kuwa ni Mbunge wa Jimbo la Hai Freeman Mbowe, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lisu, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na Mbunge wa Arusha Mjini Godbles Lema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527