DARAJA REFU ZAIDI DUNIANI LA KUPITA WATU JUU KABISA LAFUNGULIWA


Daraja lililotundikwa lenye mita 500 linalokisiwa kuwa refu zaidi duniani limefunguliwa katika mji wa Zermatt nchini Uswizi.
Daraja hilo lenye urefu wa mita 494 kwa jina Europabrucke limetundikwa mita 85 juu .
Bodi ya utalii ya Zermatt inasema kuwa ndio daraja refu zaidi duniani ,ijapokuwa daraja la mita 405 mjini Reutte Austria limetundikwa mita 110 juu kutoka ardhini.

Daraja hilo linachukua mahala pa daraja jingine ambalo lilikuwa limeharibiwa na mwamba.
Daraja hilo jipya ambalo lina uzito wa tani nane limewekwa kifaa cha ambacho kinalizuia kuyumbayumba ,kulingana na bodi ya watalii ya Zermatt.

Daraja hilo lipo kati ya Zermatt na Grachen kusini mwa Switzerland.

Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527