Picha: YALIYOJIRI KWENYE ZIARA YA RAIS MAGUFULI MTWARA...AHUTUBIA WANANCHI,ASALI ,ATUA KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mtwara katika siku ya mwisho wa ziara yake katika Viwanja vya Mashujaa mkoani Mtwara.

Wananchi wa Mtwara wakifurahia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika Viwanja vya mashujaa mkoani Mtwara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi wa Mtwara mara baada ya kumaliza kuwahutubia katika viwanja vya Mashujaa mkoani Mtwara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwaaga wananchi wa Mtwara mara baada ya kumaliza kuwahutubia katika viwanja vya Mashujaa mkoani Mtwara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kuwasili kiwandani hapo kwa ajili ya kuzindua magari 580 ya kusafirisha saruji nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kumkabidhi barua ya malalamiko kutoka kwa madereva wanaolalamikia utoaji wa ajira hizo kiwandani hapo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika viwanja hivyo vya kiwanda cha Dangote kabla kuzindua magari 580 ya kiwanda hicho yatakayosafirisha saruji nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Magari makubwa ya kusafirishia Saruji kiwanda hapo. Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote mara baada ya kukagua kiwanda chake cha Saruji mkoani Mtwara.

Mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote akimuonesha Rais Dkt. Magufuli sehemu ya Kiwanda hicho pamoja na vifaa vyake mkoani Mtwara.

Rais Dkt. Magufuli akizungumza jambo na mmiliki huyo wa Kiwanda akiwa na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Alhaji Aliko Dangote wakipeperusha bendera kuashiria uzinduzi rasmi wa Magari hayo 580.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi Mradi wa Kituo cha kupooza umeme kwa ajili ya kuusambaza katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria kuzindua kituo cha kupooza umeme kwa ajili ya kuusambaza katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wafanyakazi wa TANESCO mara baada ya kuweka jiwe la msingi la kituo cha kupooza umeme kwa ajili ya kuusambaza katika mikoa ya Lindi na Mtwara kilichopo mkoani Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia kabla ya kuweka jiwe la msingi la kituo cha kupooza umeme kwa ajili ya kuusambaza katika mikoa ya Lindi na Mtwara kilichopo mkoani Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika kituo hicho cha kupooza umeme

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika ibada ya jumapili ya kwanza ya kwaresma katika kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika ibada ya jumapili ya kwanza ya kwaresma katika kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwatakia heri waumini wa kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika ibada ya jumapili ya kwanza ya kwaresma katika kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waumini hao wa kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wanafunzi wa Shule za Sekondari mara baada ya kusali katika kanisa la Katoliki la Watakatifu Wote jimbo la Mtwara. PICHA NA IKULU

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post