Picha: HIZI NDIYO NCHI 10 ZENYE JOTO KALI ZAIDI DUNIANI

Kila nchi duniani ina sifa zake kwenye ishu ya hali ya hewa ambapo kwenye nchi nyingine kuna Joto na kwengine kuna baridi pia wengine wakiwa na hali ya hewa ya wastani, sasa leo February 7, 2017 nimekukusanyia hizi sehemu 10 zilizotajwa kuwa na kiwango kikubwa cha joto duniani.

1.QATAR

Wakati wa msimu wa joto, nchini Qatar kumeripotiwa kuwa na joto kali na kuna muda hali ya joto hupanda mpaka kufikia nyuzi joto 50 ambapo pamoja na kuwa na joto kiasi hicho Qatar imebarikiwa kuwa na utajiri mkubwa wa madini, mafuta na gesi. 

Rasilimali hizi zimeifanya Qatar kuwa nchi ya kwanza duniani kwa utajiri.



2. BOTSWANA

Botswana inashika nafasi ya pili kwa kuwa nchi yenye joto kali duniani ambalo linafika nyuzi joto 40 na inaelezwa kuwa 70% ya joto hilo huchangiwa na jangwa la Kalahari.


3. VIETNAM

Vietnam ni nchi yenye mfumo wa utawala wa Kisoshalisti kutoka bara la Asia, mji mkuu wa nchi hiyo ni Hanoi unatajwa katika nafasi ya tatu katika maeneo yenye joto kali duniani, inaelezwa kuwa kiwango cha chini cha joto ni nyuzi joto 20 wakati kiwango cha juu kinafikia nyuzi joto 42.


4. UNITED ARAB EMIRATES (UAE)

Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) unatajwa kuwa kati ya sehemu zenye uchumi unaokua kwa haraka zaidi duniani, moja ya falme zake (Abu Dhabi) inatajwa kuwa na joto linalofikia nyuzi joto 45 wakati kiwango cha chini ni nyuzi joto 25.


5. BAHRAIN

Bahrain ni moja kati ya nchi ndogo barani Asia, inatajwa kuwa joto lake hufikia nyuzi joto 40 wakati kiwango cha chini ni nyuzi joto 17.


6. JAMAICA

Jamaica inashika nafasi ya sita katika nchi zenye joto kali ikiwa na kiwango cha chini cha nyuzi joto 27.


7. MALAYSIA

Malaysia ni moja kati ya nchi za Kiislamu na mji mkuu wake ni Kuala Lumpur wakati Putrajaya ni jiji kubwa zaidi nchini humo, hali ya hewa ni joto linaloanzia nyuzi joto 25-35 mpaka kufikia nyuzi joto 40.


8. INDIA

India ni nchi ya pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu kwenye barala Asia, kiwango cha juu cha joto kinazidi nyuzi joto 48 wakati kiwango cha chini ni nyuzi joto 28, ingawa kuna maeneo ya milima hupata baridi mpaka nyuzi 1.


9. INDONESIA

Indonesia inatajwa kuwa ndio nchi kubwa ya kiislamu duniani na mji wake mkuu ni Jakarta ukiwa na visiwa vingi huku kukiwa na rekodi ya joto linalofikia nyuzi 30.


10. ETHIOPIA

Ethiopia ni nchi ya Kiafrika na mji mkuu wake ni Addis Ababa ambao unatajwa kuwa na joto linalofikia nyuzijoto 35 wakati kiwango cha chini ni nyuzi joto 25.


V

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post