Habari tulizozipata kutoka manispaa ya Bukoba mkoani Kagera zinasema kuwa kuna tetememko la ardhi limetokea na kusababisha madhara makubwa.
Tetemeko hili kubwa la ardhi linadaiwa kuwa na ukubwa wa Ritcha 5.7 limeikumbuka mikoa ya Kanda ya Ziwa hasa Kagera na Mwanza na kusababisha maafa makubwa ikiwemo nyumba za watu kubomolewa.
Maeneo yalioathirika zaidi kwa Tanzania ni, Bukoba, wilaya zote za Kagera na baadhi ya maeneo ya Mwanza. Aidha baadhi ya majeruhi ambao hawakuumia sana walitibiwa na kuruhusiwa kuondoka hospitalini hapo kurejea majumbani kwao.
Taarifa iliyotolewa na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mjini Bukoba, imeeleza kuwa watu 10 wamepoteza maisha kuokana na tetemeko hilo huku wengine zaidi ya 100 wakijeruhiwa vibaya na mpaka sasa wanaendelea kutibiwa hospitalini hapo.
ANGALIA PICHA NA SOMA HABARI KAMILI <<HAPA>>
Tazama picha nyumba zikiwa zimebomoka huko Bukoba


Social Plugin