Picha!! Mamia Wajitokeza Kuaga Mwili wa Mwendesha Bodaboda Aliyeuawa Kwa Kuchomwa Visu Kisha Kuporwa Pikipiki Shinyanga



Mamia ya wakazi wa mtaa wa Dome kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga na maeneo ya jirani wamejitokeza kwa wingi kuuaga mwili wa kijana mwendesha bodaboda Geofrey Deocres Kazinduki (24) aliyeuawa kwa kuchomwa visu mara tatu tumboni na kifuani na watu wasiojulikana kisha kumpora pikipiki yake.



Kijana Geofrey aliuawa juzi Julai Mosi saa mbili usiku katika barabara ya Shy Bush karibu na relini kata ya Maganzo wilayani Kishapu baada ya mtu asiyejulikana kumkodi kutoka katika stendi ya mabasi yaendayo wilayani mjini Shinyanga.

Inaelezwa kuwa mwendesha bodaboda huyo aliuawa na watu wasiojulikana ambao baada ya kutekeleza mauaji hayo waliondoka na pikipiki yake.

Mwili wa marehemu umeagwa leo na wakazi wa Shinyanga wakiwemo waendesha bodaboda na kesho Julai 04,2016 mwili huo utasafirishwa kwenda nyumbani kwao kijiji cha Nyakibimbili kata ya Katerelo halmashauri ya wilaya ya Bukoba Vijijini mkoani Kagera.

Marehemu ameacha mjane na mtoto mmoja.

Ibada ya kuaga mwili wa marehemu imeongozwa na mchungaji Isaack Masimango kutoka kanisa la KKKT mjini Shinyanga.

Ibada hiyo pia imehudhuriwa na diwani wa kata ya Ndembezi bwana David Nkulila

Mwandishi wa Malunde1 blog,bwana Kadama Malunde alikuwepo msibani ametuletea picha ...Tazama hapa chini
Geofrey enzi za uhai wake akiwa na bodaboda yake


Jeneza lililobeba mwili wa marehemu likiwa nyumbani kwa marehemu katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi katika manispaa ya Shinyanga

Mchungaji Isaack Masimango kutoka kanisa la KKKT mjini Shinyanga akiongoza ibada ya kuaga mwili wa marehemu Geofrey

Picha ya marehemu Geofrey

Picha ya marehemu ikiwa kwenye jeneza

Waombolezaji

Mchungaji Masimango akiombea mwili wa marehemu

Waombolezaji

Akina mama wakiaga mwili wa marehemu

Zoezi la kuaga mwili wa marehemu likiendelea

Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu

Waombolezaji

Zoezi la kuaga mwili linaendelea

Zoezi la kuaga mwili linaendelea

Zoezi la kuaga mwili wa marehemu linaendelea

Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Solomon Naringa Najulwa akiaga mwili wa marehemu,nyuma yake ni diwani wa kata ya Ndembezi David Nkulila
 
Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Solomon Naringa Najulwa akiaga mwili wa marehemu.
 
 Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Solomon Naringa Najulwa akiaga mwili wa marehemu,nyuma yake ni diwani wa kata ya Ndembezi David Nkulila

Diwani wa kata ya Ndembezi David Nkulila akiaga mwili wa marehemu

Wana mtaa wakiaga mwili wa marehemu

Zoezi la kuaga mwili linaendelea.

Dr.Ellyson Maeja akiaga mwili wa marehemu


Geofrey Tibakyenda akiaga mwili wa marehemu

Zoezi la kuaga mwili wa marehemu linaendelea






Mkurugenzi wa Malunde1 blog,bwana Kadama Malunde akiaga mwili wa marehemu


Ndugu wakisaidia mke wa marehemu wakati wa kuaga mwili wa mme wake



Ndugu wa marehemu wakiaga mwili wa marehemu


Mchungaji Dr. Meshaki Kulwa kutoka kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga akiomba wakati wa ibada hiyo



Viongozi wa chama cha waendesha bodaboda katika katika manispaa ya Shinyanga wakiwa msibani


Ndugu wakimtuliza mke wa marehemu


Waandishi wa habari wakiwa msibani


Mwenyekiti wa mtaa wa Dome Solomon Naringa Najulwa akizungumza msibani ambapo alikemea mauaji hayo na kuwataka waendesha bodaboda kuwa makini kwani kuna baadhi yao siyo waaminifu



Waombolezaji



Mwenyekiti wa waendesha bodaboda Jacob Paul akizungumza msibani ambapo aliwataka waenesha bodaboda kuepuka kubeba wateja kwenda nje ya mji kuanzia saa moja usiku


Kushoto ni diwani wa kata ya Ndembezi akizungumza msibani ambapo alisema vitendo vya kihalifu vinasimamiwa na matajiri kwani haiwezekani mtu maskini apore pikipiki,hivyo wanaofadhili uhalifu ni matajiri wenye uhakika wa soko la pikipiki


Nkulila akisisitiza waendesha bodaboda kuwa makini na kulindana


Nkulila akisisitiza jambo

Katikati ni mke wa marehemu

 Kushoto ni mjomba wa marehemu bwana  Deocres Kamara akizungumza kwa niaba ya familia



Jeneza la marehemu likiingizwa ndani kwa ajili ya safari Julai 04,2016 saa 10 alfajiri


Jeneza likiingizwa ndani ya nyumba ya marehemu
Geofrey enzi za uhai wake

Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post