Kampuni ya Mabasi ya City Boy Imefungiwa Kufanya Biashara




Siku moja baada ya kutokea ajali ya mabasi iliyosababisha vifo vya watu 30 na majeruhi kadhaa, Kampuni ya mabasi ya City Boy imefungiwa kufanya biashara hiyo kwa muda usiojulikana.


Ajali hiyo ilitokea eneo la Maweni, Manyoni, mkoani Singida baada ya mabasi ya kampuni hiyo, moja likitokea Dar es Salaam na lingine likitokea Kahama kuelekea Dar es Salaam kugongana.


Msemaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), David Mziray amesema leo kuwa kampuni hiyo ina miliki mabasi 12 na yote yamefungiwa kufanya safari yoyote kuanzia leo.


“Mabasi hayo yamefungiwa kuanzia leo kwa muda usiojulikana, ukaguzi wa mabasi yao utaanza kufanyika kupitia jeshi la polisi,” amesema Mziray.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post