Makubwa Haya!! Hasira Za Ugomvi Wa Kimapenzi Zamalizikia Kwenye Gari

Picha za gari lililokuwa na ujumbe wa kukasirisha uliochorowa katika gari hilo zimesambazwa mara elfu katika mtandao wa Twitter.

Gari hilo jeupe aina ya Range Rover Revere lenye bei ya pauni 75,000 lilionekana limeegeshwa karibu na Harrods magharibi mwa London na kuchorwa ujumbe wa kukasirisha kwa kile kilichoonekana kuwa mpenzi aliyedanganywa.

Gari hilo liliandikwa 'cheater' { mwongo} katika pande zote mbili za gari huku maneno ''Natamani angekuwa na thamani'' yakiandikwa katika madirisha ya gari hilo.

Klo ambaye alipiga picha za gari hilo alisema kuwa alimuona mwanamke mmoja akilichora gari hilo,alikuwa kama aliye na wazimu.

'Hakuna mtu aliyejaribu kumzuia.Baadaye aliondoka.Maneno ''Its Over'' pia yaliandikwa kwenye gari hilo ikielezea kuisha kwa uhusiano wowote''.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post