Rais Magufuli Kumwapisha Balozi Mteule Mheshimiwa Mathias Chikawe Leo asubuhi



Itakumbukwa kuwa leo ( jana ) asubuhi tarehe 18 Aprili, 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alimteua Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan.



Tunapenda kuwataarifu kuwa Balozi Mteule Mathias Meinrad Chikawe ataapishwa kesho (Leo) tarehe 19 Aprili, 2016 saa 3:00 Asubuhi, Ikulu Jijini Dar es salaam.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam


18 Aprili, 2016

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post