MBUNGE WA VITI MAALUM TANZANIA AFARIKI DUNIA




Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Christina Mughwai Lissu amefariki dunia kwa ugonjwa wa saratani leo.

Kaka wa marehemu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alituma taarifa kwenye mitandao ya jamii akisema amepata taarifa za msiba huo akiwa mkoani Kigoma.

Alisema Christina alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam na alianza kuugua tangu mwaka jana.

“Nawasalimu kutoka Kibondo. Nina habari zisizokuwa njema. Dada yangu aliyekuwa mbunge wetu wa viti maalumu, Christina amefariki dunia muda mfupi uliopita katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam.

“Marehemu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ‘cancer’ tangu mwaka jana. Kwa sasa niko nje ya Dar es Salaam na ndiyo kwanza taarifa hizi zimenifikia…” ilisema taarifa ya Lissu aliyoituma mitandaoni.

Christina alikuwa Mbunge wa Viti Maalumu wa Mkoa wa Singida tangu mwaka 2010 hadi 2015 na alikuwa Naibu Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha. Hakurudi bungeni katika uchaguzi wa 2015.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post