EWURA YASHUSHA BEI YA UMEME KUANZIA LEO,SERVICE CHARGE YAZIKWA




Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.



Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa.


Bei mpya kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292 toka 298 ya zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200 ya hapo awali.

Bei mpya kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152 toka sh. 156 ya hapo awali


Tazama jedwali hili kuona mgawanyo wa bei mpya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527