WATU 31 WAUAWA KATIKA UWANJA WA NDEGE NA KITUO CHA TRENI HUKO BRUSSELS




Watu 31 wamefariki baada ya mashambulio kutekelezwa katika uwanja wa ndege wa Zaventem na kituo cha treni cha Maelbeek mjini Brussels.

Waziri wa afya wa Ubelgiji amesema watu 11 walifariki na wengine 81 kujeruhiwa baada ya milipuko miwili kutokea uwanja wa ndege wa Zaventem, nje kidogo ya mji wa Brussels.

Meya wa Brussels amesema watu 20 walifariki Maelbeek.

Kundi linalojiita Islamic State limedai kutekeleza mashambulio hayo

Waziri Mkuu wa Ufaransa Francois Hollande amelaani mashambulio hayo mjini Brussels na kusema ni kama mashambulio yaliyolenga bara lote la Ulaya.

Waziri Mkuu wa Ubelgiji Charles Michel amesema hatua zaidi zimechukuliwa kuimarisha usalama mpakani.








Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527