WAZIRI MKUU FREDRICK SUMAYE AANZA KURIPUKA UKAWA- ZIKO HAPA SENTENSI ZAKE 12 TATA MKUTANO WA UKAWA JANGWANI




Sumaye: "Kama kipimo cha uadilifu ni Kinana Katibu mkuu wa CCM, basi mimi nitakuwa mtakatifu" Serikali hii ni dhaifu sana na alituthibitishia katibu mkuu, mwenyewe kusema kuna mawaziri mizigo.

Sumaye: "Lowassa angekuwa mbaya asingeteuliwa kuwa waziri mkuu, hakuna Rais anayemteua mtu mbaya kuwa waziri mkuu " Leo Lowassa ametoka CCM ameonekana hafai, lakini ni Kikwete aliemfanya waziri mkuu wake, kuna Rais anaweka kiongozi ambae hafai?

Sumaye: "Lowassa ndiye aliyemuingiza Kikwete madarakani, kama angekuwa mla rushwa asingekuwa bado yupo nchini"

Sumaye: "Lowassa alijiuzulu kumuokoa Kikwete , waziri siku zote anabeba mzigo kumuokoa "Nyerere wakati anastaafu, alisema hajaona mtu mvumilivu kama Kawawa, alibeba mizigo wa kubeba yeye, ndiyo kazi aliyofanya Lowassa.Mmewasikia kwenye kampeni, fisadi mkubwa huyo amechukua fedha za matajiri, Lowassa amechukua ustaarabu kuwajibika ili kumuokoa Rais.

Sumaye: "Lowassa ametoka madarakani miaka 8 iliyopita, hivi twiga walipopandishwa ndege Lowassa alikuwepo??"

Sumaye: "Serikali hii ni dhaifu sana, aliyethibitisha hilo ni katibu mkuu wa CCM aliposema kuna mawaziri mizigo"

Sumaye: "Wanasema eti Lowassa ni mgonjwa, kwani huyo Magufuli ni mzima??" Wanasema mgonjwa, kwani Magufuli mzima? Wanaenda kufanya nini Ulaya, mtu yeyote ukishavuka miaka 50 hauwezi kuwa wazima kwa 100%

Sumaye: "Kwani Rais Kikwete akiwa madarakani hakwenda Marekani kufanyiwa upasuaji mkubwa wa tezi dume???

Sumaye: Rais si kazi ya kubeba zege Ikulu, anatakiwa kuwake timu nzuri ya kazi, yeye ni meneja tu.
Watanzania leo elimu inashuka sana, tunashusha alama za kufaulu wanafunzi ionekane wamefaulu wengi, pia ukienda ktk afya

Sumaye: Tulitaka kufanya mabadiliko kulekule, kukawa na tatizo ndani ya CCM, ukitaka kufanya lolote wanakuzingira. 

Sumaye: Wanawajaza watanzania uoga wa usilolijua, mkiwapa wapinzani wataharibu nchi, kila binadamu ana uoga wa asilolijua.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527