WATU TISA WATEKETEA KWA MOTO JIJINI DAR ES SALAAM,ANGALIA PICHA HAPA









Familia ya watu tisa  imeteketea kwa moto katika tukio la moto uliotokea majira ya saa tisa usiku wa kuamkia leo eneo la Buguruni Malapa Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa majirani, walisikia kelele na walipoamka wakakuta moto mkubwa ukiwa unawaka katika nyumba hiyo.


Hata hivyo juhudi zao za kuvunja mlango ili kuokoa watu waliokuwamo ndani zilishindikana.

Mmoja wa mashuhuda amesema wamefanikiwa kutoa miili ya watu watano iliyoungua vibaya, na imedaiwa kuwa baba mwenye nyumba amenusurika kifo kutokana na kuwa kazini katika shifti ya usiku.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527