NIMEKUSOGEZEA PICHA 41 ZA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM SHINYANGA,MHESHIMIWA SAMWEL SITTA,LUSINDE WAUNGURUMA



Chama cha Mapinduzi wilaya ya Shinyanga mjini leo kimezindua rasmi kampeni zake za Uchaguzi mkuu ujao katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga,ambapo wabunge wa majimbo yote ya Shinyanga wamehudhuria uzinduzi huo .

Uzinduzi huo umeongozwa na waziri wa Uchukuzi mheshimiwa Samweli Sitta na mbunge wa Mtella aliyemaliza muda wake Livingstone Lusinde ambao walitumia fursa hiyo kumnadi mgombea urais wa CCM Dkt John Magufuli na kumponda mheshimiwa Edward Lowassa wakidai kuwa hafai kuwa rais kutokana ufisadi wake na kwamba Ukawa wamekurupuka kwani hawamjui vizuri Lowassa.

Makada hao wa CCM pia walisema Lowassa hana lolote zaidi ya mbwembwe na visingizio vya hapa na pale-Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog 


Wanachama wa CCM na wakazi wa Shinyanga wakifuatilia mkutano wa CCM katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga leo 


Makada wa CCM wakiwa eneo la tukio 


Mjumbe wa NEC taifa Gasper Kileo akizungumza katika mkutano huo ambazo aliwataka wanaccm kuwapuuza watu wanaozusha kuwa atahamia Chadema/Ukawa kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni rafiki yake na Lowassa,ambapo Kileo alisisitiza kuwa hajawahi na wala hafikiria kuhama CCM na kwamba CCM lazima ishinde katika uchaguzi mkuu ujao 



Wananchi wakifuatilia kilichokuwa kinajiri katika mkutano huo wa uzinduzi wa kampeni za CCM wilaya ya Shinyanga mjini 







Mheshimiwa Samweli Sitta akizungumza katika mkutano huo,ambapo aliwatambulisha wagombea ubunge majimbo yote 6 ya uchaguzi mkoa wa Shinyanga ambayo ni Ushetu,Msalala,Kahama mjini,Kishapu,Shinyanga mjini,Kishapu na Solwa na kusisitiza kuwa lazima CCM ishinde katika majimbo hayo. 



Mbunge wa viti maalum mkoa wa Shinyanga mheshimiwa Azza Hilal akiwasalimia wakazi wa Shinyanga na kuwaomba wananchi kuchagua wagombea wa CCM kwani ndiyo watawaletea maendeleo 


Wanachama wa CCM wakifuatilia kilichokuwa kinajiri uwanjani 


Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Shinyanga Lucy Mayenga akiwasalimia wakazi wa Shinyanga ambapo aliwaomba wananchi kuwapa kura wagombea wa CCM 


Mgombea ubunge jimbo la Msalala mheshimiwa Ezekiel Maige akiwasalimia wakazi wa Shinyanga wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi CCM wilaya ya Shinyanga mjini katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga 


Mgombea ubunge jimbo jipya la Ushetu mheshimiwa Elius Kwandikwa akiwasalimia wakazi wa Shinyanga ambapo ajigamba kuwa katika jimbo lake wameshamaliza kufanya uchaguzi wanachosubiri ni utaratibu tu tarehe 25 Oktoba mwaka huu. 


Mgombea ubunge wa jimbo la Kishapu mheshimiwa Suleiman Nchambi akizungumza na wakazi wa Shinyanga ambapo aliwaomba wanaShinyanga kuwapa kura wagombea wa CCM kwani ndiyo watakaowaletea maendeleo watanzania 


Mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini mheshimiwa Stephen Masele akizungumza na wakazi wa Shinyanga ambapo aliwaomba wakazi wa Shinyanga kutochagua mbunge ambaye siyo mzawa wa Shinyanga na badala yake wampe yeye kura ili kuwaletea maendeleo wananchi wa Shinyanga huku akijisifu kuwa amefanya mambo mengi ya kimaendeleo kwa wananchi katika sekta mbalimbali kama vile afya,elimu,michezo n.k 


Mheshimiwa Stephen Masele akizungumza na wakazi wa Shinyanga leo 


Mheshimiwa Samweli Sitta akiwahutubia wakazi wa Shinyanga wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi CCM wilaya ya Shinyanga mjini ambapo alisisitiza kuwa mgombea urais wa UKAWA Edward Lowassa anahusika na sakata la Richmond na utajiri wake haueleweki 


Msanii wa nyimbo za asili Madebe Jinasa akitoa burudani wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Shinyanga mjini 


Wafuasi wa CCM na wakazi wa Shinyanga wakifuatilia mkutano wa CCM leo mjini Shinyanga 


Mkutano unaendelea


Mkutano unaendelea


Mheshimiwa Livingstone Lusinde akiwahutubia wakazi wa Shinyanga ambapo alitumia muda mwingi kumponda mgombea urais kupitia Ukawa Edward Lowassa hasa kuhusu afya yake kwamba ni mgonjwa bila kutaja ugonjwa anaougua/anaoumwa 



Wanachama wa CCM wakifuatilia kilichokuwa kinajiri kwenye mkutano 


Mheshimiwa Livingstone Lusinde akizungumza mjini Shinyanga 


Wafuasi wa CCM wakiwa eneo la tukio 


Mheshimiwa Lusinde akiwaombea kura wagombea wa CCM na kumpa sifa kem kem mheshimiwa John Pombe Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia CCM 





Mkutano unaendelea 


Mkutano unaendelea 


Wananchi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea katika mkutano wa CCM leo 


Mkutano unaendelea 


Mkutano unaendelea 

Wananchi wakifurahia jambo kwenye mkutano 



Mkutano unaendelea 


Mheshimiwa Lusinde akiwahutubia wakazi wa Shinyanga 


Tunafuatilia kinachoendelea hapa..... 


Mheshimiwa Lusinde akiwa na wagombea ubunge majimbo yote ya Shinyanga,ambapo mmoja pekee wa jimbo la Solwa mheshimiwa Ahmed Salum hakuwepo kwenye mkutano huo kutokana na kuwa katika shughuli zingine za kichama 


Wabunge watarajiwa majimbo ya Shinyanga wakiwa jukwaani 


Wa tatu kutoka kushoto ni mgombea ubunge jimbo la Kahama mjini mheshimiwa Jumanne Kishimba 



Wanachama wa CCM wakicheza uwanjani 



Baada ya mkutano kila mmoja akaendelea na shughuli zake wengine wakapanda kwenye magari yao kurudi makwao 


Wakazi wa Shinyanga wakiwa eneo la mkutano 


Wazee wa CCM wakiwa eneo la tukio 

Vijana wa Greenguard wakiwa eneo la tukio 

Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527