Mpya Kabisa!!! DIAMOND PLATNUMZ APATA TUZO YA UZAZI!!!


Msanii wa Bongo mwenye umaarufu wa kimataifa, Diamond Platnumz, maarufu, Naseeb Abdul, amepata majukumu mapya baada ya kujaliwa mtoto.

Mkewe msanii huyo, Zarina Hassan, Zari the boss lady, alijifungua msichana mapema leo na kuipa furaha familia hiyo.

Baada ya kuokota tuzo tofauti kwenye mziki, Diamond hatimaye amepata tuzo kutoka kwa Mungu kwa kufanya juhudi nyingi za kutaka kuwa mzazi.

Diamond alipachika picha ya mtoto wake akibebwa na mamake, Sanura Kassim kwenye ukurasa wake wa Instagram na kupokea pongezi kutoka mashabiki.

Aidha, msanii huyo amemuanzishia mtoto wake ukurasa wa Instagram kwa jina Tiffah Dangote na kuvutia zaidi ya wafuasi elfu kumi na sita.

Diamond mwenye umri wa miaka 25, aliwashangaza wengi kwa kuanza kumfanyia bintiye ununuzi wa vifaa vya watoto kabla ya kuzaliwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post