Breaking News!! LOWASSA ATANGAZA RASMI KUIPIGA CHINI CCM NA KUHAMIA CHADEMA,ASEMA CCM SIYO MAMA YAKE..


Waziri Mkuu aliyejiuzuru, Edward Lowassa amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), leo Jijini Dar es salaam


Baada ya Uvumi wa muda mwingi na kitendawili kilichokuwa kigumu kukitegua juu ya waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa kwamba wapi anahamia kama ilivyokuwa ikiandikwa katika vyombo vya habari kwamba anajiunga na Ukawa,Hatimaye leo hii ametegua kitendawili hicho Baada ya kutangaza kwa kinywa chake kuwa sasa amejiunga na chama kikuu cha upinzani cha demokrasia na maendeleo CHADEMA.

Hatua hiyo sasa inamaliza uvumi kuhusu hatma ya kiongozi huyo baada ya kuondolewa katika uteuzi wa mgombea wa urais wa chama cha CCM,ambapo amesema kuwa hajakurupuka kwa uamuzi huu, anawaomba Watanzania wajiunge na UKAWA katika Safari ya Matumaini na kusema”Watanzania wanataka mabadiliko wakikosa ndani ya CCM watayapata nje ya CCM.”Kauli aliyosema Mwalimu nyerere enzi za uhai wake.



Hizi ni baadhi ya sentensi alizotamka
 Lowassa: Namshukuru mke wangu Regina, wanangu na wanafamilia katika kipindi hiki kigumu kilichojitokeza.

Lowassa: Nawashukuru wanaCCM waliojitokeza kuniunga mkono wakati nikitafuta wadhamini.


Lowassa: Kilichotokea Dodoma, ni kupora madarakani ya kamati kuu, waswahili wanasema kubaka demokrasia.

Lowassa: Chuki na roho mbaya zilitawala licha ya mimi kuwa mgombea mwenye ushawishi na anayekubali zaidi kuliko wote.

Lowassa:Kwa mantiki hii nitakuwa mnafiki kama nitaendelea kudanganya nafsi yangu na Watanzania kuwa bado nina imani na CCM.

Lowassa: Sijakurupuka kwa uamuzi huu, nawaomba watanzania wajiunge na UKAWA katika Safari ya Matumaini.


Lowassa: Wanaoogopa kisasi wamefanya madhambi gani? Waulizeni..mimi ni Mkristo,sina kisasi..waende wakatubu kwa Mungu wao.

Lowassa: CCM Si baba yangu wala Mama yangu. Watanzania kama wameyakosa mabadiliko ndani ya CCM, basi watayapata nje ya CCM.

Lowassa: CCM ninayoiona Dodoma siyo iliyomkuza..
"CCM siyo Mama Yangu,Nahama CCM nahamia Ukawa kupitia Chadema,watanzania wanahitaji mabadiliko wasipoyapata ndani ya CCM watayapata nje ya CCM  na sio kwingine bali ni Ukawa".

Lowassa hatimaye amemaliza rasmi kujiunga na CHADEMA na baada ya kutangaza watu wakaanza kushangilia wakiimba
'Tunaimani na Lowassa, oya oya'


Lowassa Amesema hajakurupuka kwa uamuzi huu, awaomba Watanzania wajiunge na UKAWA katika Safari ya Matumaini

Kuhusu Ufisadi Richmond 
Lowassa: "Kila siku Richmond,Richmond...mwenye ushahidi peleka mahakamani,kama hauna Keep quiet,acha kupiga piga kelele!!"

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527