Hii Kali!! MACHANGUDOA WA KAHAMA WATUMIA NYAMA YA NGURUWE (Kitimoto) BADALA YA ARV KUPUNGUZA MAKALI YA UKIMWI



Idadi kubwa ya wanawake wanaofanya biashara ya ngono Mjini Kahama wamedaiwa kugoma kutumia dawa ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi licha ya kupima na kubainika wanaishi na maambukizi ya ugonjwa huo badala yake hutumia kula nyama ya kitimoto kwa madai inapunguza kasi hiyo kuliko dawa za ARV.

Hali hiyo imeelezwa jana Mjini Kahama na afisa maendeleo ya jamii Mjini Kahama Fanuel Ruben ambaye amesema ofisi yake imefanya ukaguzi kwenye madanguro yanayotumiwa na wanawake hao kwa biashara ya ngono na kubaini wapo wasichana kati ya miaka 15 hadi 20.

Ruben amesema baada ya kubaini hiyo wamewachukua wasichana na kuwafanyia vipimo wengi wao wamebainika kuwa na ujauzito na maambukuzi ya virusi vya ukimwi hali iliyoonyesha wanafanya ngono bila kutumia kinga ya maambukizi ya magonjwa ya kuambukiza.


Hata hivyo amesema wasichana hao baada ya kuwafanyia uchunguzi wamegoma kutumia dawa za kupunguza makali kwa madai wenzao wanaoishi na virusi vya ukimwi hutumia nyama ya kitimoto badala ya dawa hiyo.

Kufuatia hali hiyo Ruben amesema ameandaa mkakati wa kuwachukulia hatua wale wote wanaofanya biashara ya ngono huku wakijua wao ni waathirika wa ugonjwa huo kwa kuwa ipo sheria mpya inayokataza mwathirika wa virusi vya ukimwi kuwaambukiza wenzake kwa makusudi.

Kauli hiyo imekuja baada ya mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya kutangaza msako wa kuyafunga madanguro yote yanayotumiwa na wanawake hao kwa biashara ya ngono baada ya kubainika wengi wa wateja wao ni vijana wadogo ambao wanahatarisha maisha yao.
Via>>Kijukuu Blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post