Kimenuka!! MIKOROGO YAPIGWA MARUFUKU!! WANAOJICHUBUA WAIKOROGA SERIKALI



   

Nchi ya Ivory Coast imepiga marufuku uigizwaji uuzaji na usambazaji wa bidhaa zozote zenye uwezo wa kuchubua rangi ya ngozi ya binadamu .
Katika taarifa kwa vyombo vya habari Wizara ya afya imetangaza kuwa ni haramu kuingiza bidhaa hizo katika namna yeyote iwe ni vipodozi ama matembe kwa sababu ya athari zake kwa afya.
http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/05/hili.jpg
Bidhaa nyingi za kijichubua rangi ya ngozi zinauzwa katika taifa hilo la Magharibi mwa Afrika.
Marufuku hiyo inaharamisha uingizwaji wa vipodozi ,mafuta, na tembe zenye madini ya zebaki na vyuma vinavyotumiwa kuchubua rangi pamoja na kemikali zingine nyinginezo.

Mwanamke aliyetumia ''Mkorogo''
Kulingana na afisa wa halmashauri inayosimamia matumizi ya madawa nchini humo Christian Doudouko,
Idadi ya watu ambao sasa wanaonesha  za kuathirika kiafya na madawa hayo ya kuchubua ngozi imeongezeka mno katika miaka ya hivi punde na kulazimisha wizara ya afya kuchukua hatua hiyo kali.
Afisa huyo aidha alisema kuwa madini hayo haswa Zebaki yanaweza kusababisha maradhi ya saratani ya ngozi.



Daktari Elidje Ekra alisema kuwa kemikali zinazotumika ilikuhakikisha ufanisi wa kuchubua rangi asili ya binadamu zinachangia pakubwa kuzuka kwa matatizo ya shinikizo la damu pamoja na hata Kisukari.
Daktari Ekra ambaye ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Treichville Abidjan anasema ameshuhudia magonjwa mengi tu ya ngozi yasiyo na tiba na kila alipofanya upelelezi aligundua kuwa wagonjwa walikuwa pia ni watumizi wa mikorogo.
Mikorogo hiyo ya kujichubua ngiozi na maarufu mno katika mataifa mengi ya Afrika huku wanawake wengi wakipendelea kujichubua iliwakubaliwe kuwa ni warembo.

Senegal imeanza kampeini ya kupinga ''mikorogo''
Kasumba hiyo ikichochewa na dhana kuwa mwanamke mrembo sharti awe na ngozi laini na nyeupe.
Matumizi ya mikorogo sasa hata imeanza kupata umaarufu miongoni mwa wanaume.
Licha ya kutokuwepo na takwimu maalum kuhusu matumizi ya mikorogo hiyo, mabango ya mauzo na kunadi bidhaa zenye uwezo wa kukufanya uwe ''Mrembo'' zimezagaa kote barani Afrika.
Haijajulikana hadi sasa wanawake wanaozitumia wamelichukulia vipi kauli hiyo ya serikali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post