Utawala nchini Nepal unasema kuwa
watu zaidi ya watu 4000 wamedhibitishwa kuaga dunia huku wengine 8000
wakijeruhiwa kwenye janga la tetemeko la ardhi lililosababisha uharibifu
mkubwa siku ya Jumamosi.
Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa kipimo cha richta 7.8.
Jitihada za uokoaji zinaendelea kukiwa
na matumaini ya kuwapata manusura, lakini jitihada hizo bado
hazijayafikia maeneo mengine yaliyo mbali.
Watu wengi walilala nje kwa usiku wa tatu mfululizo kwenye mji mkuu Kathmandu wakihofia kutokea kwa mitetemeo mingine midogo.
Serikali
ya Nepal inasema kuwa inahitaji kila msaada ukiwemo wa mablanketi ,
helkopta, madaktari na madereva. Kuna uhaba wa maji , chakula na umeme
huku kukiwa na hofu ya kutokea kwa milipuko ya magonjwa.
Via>>BBC
Angalia Picha hali halisi ilivyo
Hali ya barabara
Via>>BBC
Angalia Picha hali halisi ilivyo
Hali ya barabara