Inatisha Sana !!WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI HUKO NEPAL YAFIKIA 4000, MAJERUHI 8000,PICHA ZIKO HAPA

Eneo la mji wa Kathmandu baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi 

Utawala nchini Nepal unasema kuwa watu zaidi ya watu 4000 wamedhibitishwa kuaga dunia huku wengine 8000 wakijeruhiwa kwenye janga la tetemeko la ardhi lililosababisha uharibifu mkubwa siku ya Jumamosi.

Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa kipimo cha richta 7.8.

Jitihada za uokoaji zinaendelea kukiwa na matumaini ya kuwapata manusura, lakini jitihada hizo bado hazijayafikia maeneo mengine yaliyo mbali.

Watu wengi walilala nje kwa usiku wa tatu mfululizo kwenye mji mkuu Kathmandu wakihofia kutokea kwa mitetemeo mingine midogo.

Serikali ya Nepal inasema kuwa inahitaji kila msaada ukiwemo wa mablanketi , helkopta, madaktari na madereva. Kuna uhaba wa maji , chakula na umeme huku kukiwa na hofu ya kutokea kwa milipuko ya magonjwa.

Via>>BBC
Angalia Picha hali halisi ilivyo

Wafanyakazi wa uokozi kutoka Japan wakiwasili Kathmandu

Wafanyakazi wa uokozi kutoka Japan wakiwasili Kathmandu


Hali ya barabara
Watu wakiwa wamelala mitaani baada ya tetemeko la ardhi 
Watu wakiwa wamelala mitaani baada ya tetemeko la ardhi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527